×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands of Readers
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Polisi watoweka baada ya kuvamiwa na washukiwa wa Al Shabaab

Living

Na Beatrice Maganga Maafisa wanne wa polisi wanaohudumu katika Kituo cha Polisi cha Hamey kwenye mpaka wa Kenya na Somalia wameripotiwa kutoweka baada ya kituo chao kuvamiwa na washukiwa wa kundi gaidi la Al Shabaab. Washukiwa hao wameripotiwa kutoweka na bunduki kadhaa pamoja na gari la polisi wakati wa uvamizi huo uliotekelezwa usiku wa kuamkia leo. Maafisa wawili aidha walijeruhiwa vibaya kwenye kisa hicho na tayari wamesafirishwa kwa ndege hadi Nairobi kwa matibabu zaidi. Walioshuhudia kisa hicho wanasema wavamizi hao vilevile walitoweka na sare za polisi. Maafisa zaidi wametumwa katika kituo hicho huku doria ya angani na ardhini ikiimarishwa kuwasaka wahusika wanaoaminika kutoroka na kuingia Somalia.

 

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week

.

Similar Articles

.

Recommended Articles