Mbunge wa Malindi Aisha Jumwa amepata afueni baada ya Mahakama Kuu ya Mombasa kutupilia mbali kesi iliyowasilishwa ya kuitaka kumzuia kugombea Ugavana wa Kilifi, Agosti 9.Jaji Stephen Githinji ametupilia mbali kesi hiyo akisema kwamba mahakama yake haina mamlaka ya kuishughulikia.Juma amesema walalamishi kwanza walipaswa kuwasilisha malalamishi yao kwa Kamati ya Tume ya Uchaguzi IEBC ya kusuluhisha mizozo kabla kuelekea mahakamani.Wapiga kura kadhaa katika Kaunti ya Kilifi wakiwamo Daniel Chengo, Rajab Menza na Karl katingu walikuwa wamewasilisha maombi matatu tofauti mbele ya mahakama hiyo kupinga uteuzi na kuchapishwa kwa jina la Jumwa katika gazeti rasmi la serikali kuwa mgombea wa UDA katika kinyang’anyiro cha Ugavana wa Kilifi.Kulingana nao Jumwa hakuafiki vigezo vinavyohitajika vya kuwania wadhifa huo kwani hana cheti cha degree kutoka kwa tasisi ya elimu inayotambulika humu nchini.Walalamishi hao pia waliegemeza kesi yao kutokana na ripoti ya tathmini ya dhamana iliyowasilishwa mahakamani tarehe 22 mwezi wa Oktoba mwaka 2020 ambayo walidai ilithibitisha kwamba Jumwa hajawahi kutunukiwa shahada.Kupitia wakili wao Derick Odhiambo pia walidai kwamba Jumwa hakuwasilisha stakabadhi halili za masomo alipofika mbele ye IEBC kuidhinishwa.Katika kesi hiyo washtakiwa wengine walikuwa IEBC, Tume ya Elimu ya Chuo Kikuu CUE, Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi EACC na Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Uongozi International Leadership University.Jumwa atamenyana na Gideon Mung’aro wa ODM, George Kithi wa PAA, Dzombo Mbaru wa Chama cha Safina na wagombea wengine wawili wa binafsi Michael Tinga na Francisco Esposito anayetambuliwa kwa jina maafuru Kasoso wa Baya.
Furaha kwa Jumwa mahakama ikimruhusu kuwania ugavana Kilifi
News
By Robert Menza| 1yr ago | 1 min read
.
Trending Now
- Renowned activist Asunta Wagura welcomes twins at 60
- How KMPDC handles cases of malpractice and negligence
- The journey to being a doctor is not for the poor or faint-hearted
- Teachers at the forefront of getting girls vaccinated against deadly virus
- Patients agony as doctors in public hospitals hustle in private practice
- Let's recommit to strategies for malaria-free, equitable world by 2030
- Struggles of a mother with an intersex child
- HIV kits donation saga brews as ministry, manufacturer differ
- Medics: No amount of threats will force us to end the strike
- Uhuru: I feel betrayed, but that is all politics
.
Popular this week
- Renowned activist Asunta Wagura welcomes twins at 60
- How KMPDC handles cases of malpractice and negligence
- Patients agony as doctors in public hospitals hustle in private practice
- The journey to being a doctor is not for the poor or faint-hearted
- Medics: No amount of threats will force us to end the strike
- Gachagua calls for dialogue with independent offices
- Property developers shy away from new projects in Nairobi
- Uhuru: I feel betrayed, but that is all politics
- Mary J. Blige on a mission to help women discover their strength
- Serb majority in N.Kosovo shuns vote on ethnic Albanian mayors
Previous article
.
Similar Articles
.
Latest Articles
Health & Science
2024-04-30 17:00:00
Health Opinion
2024-04-30 13:17:27
Health & Science
By Rosa Agutu
2024-04-29 20:50:00
.