×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Sitajiuzulu. Asema, Mwenyekiti wa EACC Philp Kinisu

Living

Na Carren Omae Kufuatia madai ya Ufisadi ambayo yameanza kumwnadama Mwenyekiti wa Tume ya Maadili na Kukabili Ufisadi Philip Kinisu, amesema hatojiuzulu. Akiwahutubia wanahabari Jumanne asubuhi, Kinisu amesema iwapo atafanya huenda kuna watu ambao wakatumia njia za kutoa madai kuwashinikiza maafisa wa serikali kujiuzulu nyadhfa zao. Amesema kuna watu wenye ushawishi na ambao wanachunguzwa na EACC na ambao wameanza kutumia madai hayo kukandamiza uchunguzi dhidi yao. Suala hilo linahusiana na malalamishi yaliyoibuliwa na Shirika moja kwa jina Bunge la Wananchi, ambao walilalamika kwamba kampuni moja inayohusishwa na Kinisu ilihusika katika biashara ya mamilioni ya pesa na NYS , ambayo inachunguzwa na EACC inayoongozwa na Kinisu. Hata hivyo Kinisu amesema kampuni hiyo ilianza kufanya kazi kabla yake kuteuliwa katika wadhfa anaoushikilia sasa huku akisema suala hilo linachunguzwa na idara kadhaa na wala sio EACC pekee. Tayari, EACC imetangaza kwamba kundi la wataalam linashughulikia malalaishi yaliyoibuliwa dhidi ya Mwenyekiti wake huku Kinisu akisema yuko tayari kushirikiana na wachunguzi.

 

Related Topics


.

Similar Articles

.

Recommended Articles