×
App Icon
The Standard e-Paper
Read Offline Anywhere
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Polisi wafutwa kazi baada ya wafungwa kutoroka gerezani

Living

Na, Carren Omae

Idara ya Magereza imewaachisha kazi kwa muda maafisa wanane kufuatia kisa ambapo wafungwa wanne walitoroka kutoka gereza la Kibos Mjini Kisumu. Miongoni mwa waliofutwa kazi kufuatia uchunguzi wa awali ni afisa aliyekuwa kazini kisa hicho kilipotokea. Kamanda wa Idara ya Magereza eneo la Nyanza, Amos Misik amesema maafisa hao wameachishwa kazi ili kutoa nafasi ya uchunguzi kufanywa. Hayo yanajiri huku polisi mjini humo wakiendelea kuwasaka wafungwa hao. Mkuu wa Polisi eneo hilo, Joseph Keitany amesema wanne hao walikuwa wakizuiliwa kwa tuhuma mbalimbali na kwamba msako dhidi yao unaendelea. Waliotoroka ni Douglas Onyancha, ambaye vilevile anakabiliwa na mashtaka ya Kumuua mfungwa mwenzake katika gereza la Kodiaga. Wengine ni Kennedy Wesonga, Keneth Lekesho na Salim Sifuna kwa jina jingine, Masibo.

 

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week

.

Similar Articles

.

Recommended Articles