Ziwa Nakuru ni maarufu kwa maelfu ya ndege aina ya flamingo, na ndicho kivutio kikubwa cha watalii nchini Kenya lakini katika miaka ya hivi karibuni, kupungua kwa idadi ya ndege hao kumeshuhudiwa, ambapo wataalamu wanasema hali hii imesababishwa na ongezeko la maji ziwani humo na kuchangia ukosefu wa chakula. Kwa sasa wanasayansi wameanzisha mchakato wa kutafuta chakula mbadala kuwasaidia ndege hao aina ya flamingo.
Katika ziara ya Radio Maisha katika mbuga ya wanyama ya Ziwa Nakuru katika halfa ya Wanahabari iliyoandaliwa na Taasisi Inayoshughulikia masula ya mazingira Sayansi Afya na Kilimo yaani Media for Environment, Science, Health and Agriculture in Kenya (MESHA) tulipata maelfu ya ndege hawa aina ya flamingo wakielea na kutambaa juu ya ziwa, wakipaka ukingo wa Kusini mwa Ziwa rangi ya waridi. Ziwa Nakuru limeorodheshwa kuwa mojawapo la maziwa yenye kupendeza zaidi duniani, na kivutio chake maarufu kikiwa ni ndege hawa aina ya flamingo.
Facts First
Unlock bold, fearless reporting, exclusive stories, investigations, and in-depth analysis with The Standard INSiDER subscription.
Already have an account? Login
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.