Naibu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, IEBC Juliana Cherera amewasilisha majibu yake kuhusu kesi ya kupinga ushindi wa Rais Mteule, William Ruto. Cherera amedai kwamba kulikuwa na aina mbili za fomu 34A nyingine ambayo Cherera amesema haikuwa halali. Pia amedai kwamba matokeo katika maeneo mbunge 27 hayakuthibitishwa kabla ya kutangazwa. Amesema matokeo yaliyotangazwa na Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati yalikuwa yake binafsi wala si matokeo ya tume.
Mbali na hayo amedai kwamba tangu wateuliwe katika IEBC pamoja na makamishna wengine ambao ni Justus Nyang'aya, Irene Masit na Francis Wanderi hawajakuwa wakihusishwa ifaavyo katika kufanya maamuzi mbalimbali.
Cherera amedai kwamba Chebukati amekuwa akiwahamisha maafisa wa uchaguzi bila kuwahusisha makamishna vilevile kutofanya mkutano wa kujadili namna ya kutekeleza mapendekezo ya kampuni ya KPMG iliyofanya ukaguzi wa sajili ya wapiga-kura.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.