Shule zote nchini zitafungwa kwa muda kuanzia tarehe 6 mwezi Agosti ili kupisha shughuli ya uchaguzi mkuu wa wiki ijayo.
Akizungumza katika Shule ya Upili ya Alliance, Waziri wa Elimu Profesa George Magoha amesema shule zitafungwa kwa siku 9 hadi Agosti tarehe 15 kwa kuwa nyingi zinatumika kama vituo vya kupigia kura.
Hata hivyo amesema iwapo kutafanyika duru ya pili ya uchaguzi wa basi shule zitasalia kufungwa hadi ikamiike. Amesema maandalizi ya mitihani ya kitaifa ambayo imeratibiwa kufanyika Novemba mwaka huu yanaendelea akisema iwapo shughuli za masomo zitaathirika sana na uchaguzi mkuu, basi washikadau katika sekta ya elimu watafanya jadiliano iwapo mitihani hiyo itafanyika au itaahirishwa.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.