Na, Beatrice Maganga/ John Mbuthia Rais asema hakuona umuhimu wa kuhudhuria mjadala wa urais Siku moja baada ya kukosa kuhudhuria mjadala wa urais, Rais Uhuru Kenyatta leo hii ameendeleza kampeni kwenye Kaunti za Murang'a na Nyeri huku akichukua fursa hiyo kufafanua sababu za kutohudhuria mjadala huo. John Mbuthia ameifuatilia ziara hiyo ya Rais na hii hpa taarifa yake. Akihutubu katika eneo la Mukurweni ambalo hakulizuru awali wakati wa ziara yake siku chache zilizopita, Rais Kenyatta amesema alikosa kuhudhuria mjadala kwa kuwa haukona haja ya kufanya hivyo akisema maendeleo aliyowafanyia wananchi yako bayana Uhuru ambaye amesema alimtazama Raila katika runinga wakati wa mjadala huo, amemshtumu kwa kusema hakuwa na mamlaka ya moja kwa moja ya kukabili ufisadi alipokuwa katika serikali ya mseto. Rais Kenyatta aidha hakukosa kuvishtumu vyombo vya habari akisema havijakuwa vikimuunga mkono tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2013.Rais Kenyatta ameendeza ziara maeneo ya Tetu na kuwaahidi wakazi kwamba atabuni kata mpya eneo hilo. Katika Eneo Bunge la Othaya, Rais ameahidi kufunguliwa kwa hospitali ya Rufaa ya Othaya Februari mwaka ujao huku huduma za akina mama kujifungua bila malipo zikiendelea kuboreshwa. Naibu wa Rais, William Ruto ambaye ameendeleza kampeni kwenye kaunti za Vihiga na Kakamega kwa upande wake ameyakosoa madai ya Raila kuwa kuna njama ya kuwahusisha maafisa wa usalama katika kufanikisha udanganyifu wakati wa uchaguzi mkuu.
Rais asema hakuona umuhimu wa kuhudhuria mjadala wa urais
Living
By | 8 years ago | 1 Min read
.
Trending Now
- Ground rules that ladies forget when dating
- How you can stay pregnant and fabulous
- Top hotels in city fully booked for Obama visit
- The burning truth: Crucial facts about UTIs that you need to know
- Clash of new and old homes in Kisumu’s Tom Mboya
- Do you need to shower every day?
- How State electricity firm paid Sh430m for fraudulent projects
- Achieving woman: ‘Lawyer’ grandma helps youth keep off poaching
- No more cooking and cleaning, you’re his girlfriend, not a wife!
- Signs that may show you have Endometriosis and you are not aware
.
Popular this week
- Easy recipe: Walnuts cheesy kunafa
- Playing favourites: The 'golden child' of the family
- Why Kisiis unapologetically roast ‘witches’
- Quiet strength of mothers raising kids with special needs
- Elevate your graphic T-shirt into a fashion statement
- How to report a superior without risking your job
- Delicate dance: What reciprocity really looks like in relationships
- What Kenyan women want from their men
- MPs demand end to delocalisation of teachers
- Fathers must help kids discover talent
.
Similar Articles
.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.