×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Kesi ya mwenyekiti wa SONU ya ahirishwa

Living

Na, Suleiman Yeri

Mahakama ya Milimani siku ya Jumatatu imeahirisha kusikilizwa kwa kesi ya uchochezi dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Nairobi, SONU Babu Owino hadi tarehe 15 Oktoba. Hakimu Mkuu wa Mahakama hiyo, Kennedy Cheruiyot ameiahirisha kesi hiyo baada ya upande wa mashtaka kusema mashahidi wake wakuu wasingeweza kufika mahakamani leo hii. Wakati uo huo, Wakili wa Owino amesema hakuwa tayari kuendelea na kesi hiyo kwa vile hajapokea nakala muhimu kutoka upande wa mashtaka zikiwamo taarifa za mashahidi. Inadaiwa kuwa mnamo Juni 13 mwaka huu, katika Makao Makuu ya Chama cha ODM, Owino alitoa matamshi ya chuki dhidi ya Mbunge wa Gatundu Kusini, Moses Kuria. Mshtakiwa aliachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu shilingi laki moja au bondi ya shilingi laki tano akisubiri kusikizwa na kuamuliwa kwa kesi dhidi yake.  

 

Related Topics


.

Similar Articles

.

Recommended Articles