×
App Icon
The Standard e-Paper
Read Offline Anywhere
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Kesi kuhusu digri ya Sakaja yaanza kusikilizwa

Living

Mawakili wa Seneta wa Nairobi Jonson Sakaja wamepuuza hoja kwamba picha za sherehe ya kufuzu kwa Sakaja, zinafaa kutolewa ili kutumika kuthibitisha uhalali wa digrii yake.

Aidha, upande wa utetezi umesema si lazima kwa Sakaja kutoa stakabadhi zote za kubainisha iwapo alisoma mwaka wa 2017 katika Chuo Kikuu cha Team nchini Uganda ama la, na kwamba ni porojo kwa yeyote kupinga uhalali wa digri yake kwa msingi huo.

Sakaja kupitia mawakili wake, akiwamo Elias Mutuma, amepongeza uamuzi wa Kamati ya Kusuluhisha Mizozo katika Tume ya Uchaguzi IEBC, wa kumwidhinisha kuwania ugavana kupitia chama cha UDA

Aidha, Wakili Mutuma amekosoa ushahidi wa upande wa mlalamishi kupinga ugombea wa Sakaja, akisema ushahidi huo unajumuisha maneno ya kusikia tu bila uhakika.

Jaji Anthony Mrima wa Mahakama Kuu ya Milimani ameanza kusikiza kesi hiyo Jumatatu, ambayo iliwasilishwa na mlalamishi Dennis Wahome, anayeshinikiza Tume ya Uchaguzi IEBC kutochapisha jina la Seneta Sakaja katika karatasi za kupigia kura.

Wahome kupitia Wakili Njoki Mboce, anaitaka mahakama hiyo kutupilia mbali uamuzi wa IEBC kumwidhinisha Sakaja.

Alhamisi iliyopita, Tume ya Elimu ya Vyuo Vikuu ilibatilisha uhalali wa digrii ya Sakaja.

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week

.

Similar Articles

.

Recommended Articles