×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Tatizo li wapi, Sudan Kusini?

Living

Ni wiki ya pili sasa, mapigano yanaendelea nchini Sudan Kusini. Zaidi ya watu 300 wamefariki

dunia. Sio raia wa taifa hilo pekee walioathirika bali wa mataifa mbalimbali. Swali langu ni je,

Sudan Kusini tatizo li wapi? Ni miaka mitano tu baada ya kujipatia uhuru kutoka Sudan, kilio

cha mwanzo kilikuwa ni unyanyasaji kutoka kwa taifa linaloongozwa na Omar al Bashir lakini

kwa mtazamo wangu ilivyo sasa yapo zaidi yanayoibua hisia baina ya wananchi na kutoelewana

kati ya rais Salva Kiir na makamu wake Riek Machar.

Nawazia hivi, viongozi wetu wa Afrika wakati umewadia kuweka maisha ya wananchi mbele

na kufikiria uchumi wa matiafa yetu. Sio jambo la busara kuwaona tunaowaita viongozi kuwa

ndio wa kuwapiganisha wananchi. Nina hakika mapigano hayo yanapoendelea viongozi hao

mashuhuri wana walinzi, askari waliopokea mafunzo ambao hujitolea kwa hali na mali

kuwalinda wakubwa wao, lakini wananchi je?

Wengi hujikuta katika kambi za wakimbizi hasa katika mataifa jirani, hali ya maisha katika

kambi hizo ni ngumu, wengi hufariki hata kabla ya kupata makao mbadala, nani wa kuwajali?

Kwa mfano Kenya ina wakimbizi wengi kutoka Sudan Kusini. Ingawa idadi yao ni kubwa, kuna

wengi waliosalia kuteseka nchini mwao na wengine ambao wameangamia kutokana na

makombora ya pande hasimu.

La kushangaza ni kwamba taifa hilo lina utajiri mkubwa wa raslimali, kama vile mafuta.

Viongozi hawa wangaliketi nchini na kufanya mazungumzo lingekuwa taifa

ambalo linatamaniwa kote ulimwenguni.

Anavyosema muhariri wangu ''haiwezekani kuwaweka maadui wawili wakalala pamoja, mmoja

anaweza kumuua mwezake kabla ya machweo''. Je, ndiyo hali ya Machar na Kiir? Viongozi

hawa ni maadui ambao hawawezi kuelewana kwa ajili ya taifa changa zaidi ulimwenguni? Kama

ni hivyo basi, taasisi zenye mamlaka zaidi katika ukanda huu kama vile Umoja wa Afrika,

Jumuiya ya Afrika Mashariki na mamalaka ya maendeleo katika ukanda huu, IGAD zinafaa

kuwachukulia hatua madhubuti wawili hao. Wanafaa kuwajibishwa ili warejeshe amani na

kuidumisha la sivyo waongozwe kuwapa wengine wanaojali raia fursa ya kuongoza. Kwa sababu

ukosefu wa usalama katika taifa hilo, bila shaka utayakosesha usingizi mataifa jirani Kenya

ikiwamo.

Carren Omae, Ripota Radio Maisha

[email protected] [email protected]

Twitter: @CallenOmae

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week

.

Similar Articles

.

Recommended Articles