×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

IEBC yafanya majaribio kuhusu mitambo ya uchaguzi

Living

Na, Beatrice Maganga IEBC yafanya majaribio kuhusu mitambo ya uchaguzi Hatimaye Tume ya Uchaguzi, IEBC imeifanyia majaribio mitambo ya kutuma matokeo ya uchaguzi kwa njia ya kielektroniki katika ukumbi wa Bomas, jijini Nairobi, kituo kikuu cha kujumlisha kura. Majaribio hayo yamehusu kuyapokea matokeo kutoka vituo mbalimbali nchini ambavyo vimehusishwa katika mpango huo wa majaribio. Ni sauti ya mmoja wa maafisa wa IEBC akieleza utaratibu wa kuyapokea matokeo ya uchaguzi kutoka vituo mbalimbali vya majaribio. Matokeo hayo yalitandazwa katika mashine kubwa huku majina na picha za wawaniaji urais yakiwekwa katika mashine hiyo. Punde matokeo yanapowasilishwa na maafisa katika vituo mbalimbali kwenye kaunti, yanatandazwa katika mashine hiyo huku yakionesha idadi ya kura za kila mwaniaji. Aidha majina ya kaunti zote yameorodheshwa huku kukiwa na uwezekano wa kufuatilia matokeo ya kila kaunti kwa kubonyeza jina la kaunti inayohusika. Mwenyekiti wa IEBC, Wafula amefafanua hatua ambazo zinastahili kuchukuliwa iwapo kuna tofauti za matokeo katika mashine na yale yaliyotangazwa na afisa wa uchaguzi katika kituo. Afisa Mkuu Mtendaji wa IEBC, Ezra Chiloba aidha amesema vituo vyote vikuu vya kupeperusha matokeo ya uchaguzi vitakuwa vikipeperusha matokeo sawa huku ukiwapo wavuti maalum ambao mtu anaweza kutumia kufuatilia matokeo. Licha ya kupeperushwa kwa matangazo hayo kwa njia ya kieleketroniki wakati wa uchaguzi mkuu, Chebukati amesema kuna vituo thelathini na vitatu ambavyo matokeo yatawasilishwa kwa mfumo usio wa kielektorini kutokana na hali kwamba maeneo mengine majina ya wawaniaji zaidi yalijimuishwa dakika za mwisho kutokana na maamuzi ya mahakama hivyo majina yao hayako katika data za awali. Chebukati aidha amesema karatasi za kura kwenye maeneo mengine aidha zitachapishwa upya baada ya kujumuishwa kwa majina ya wawaniaji wengine dakika za mwisho. Kampuni za mawasiliano za Safaricom, Airtel na Telkom zitashiriki shughuli ya upeperushaji wa matokeo ya uchaguzi, tofauti na uchaguzi uliopita ambapo kampuni moja tu ya mawasiliano ilitegemewa. Hayo yanajiri huku shughuli ya kuapishwa kwa maafisa elfu mia tatu sitini watakaosimamia uchaguzi mkuu na maajenti wa wawaniaji wakiapishwa rasmi.

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week

.

Similar Articles

.

Recommended Articles