Uteuzi wa Makatibu Wazua Tumbojoto, Raila akitaka Waluke Kuachiliwa | Siasa na Gumzo Podcast
Published Nov. 05, 2022
00:00
00:00

Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu ya Tinga Kenya Kwanza, Tinga naye anasema wewe kijana wacha kuniota kila saa mimi si rika lako. Unamshauri vipi Riggy G? Vilevile Baba anataka Waluke kuachiliwa huru. Eti kesi dhidi yake itupiliwe mbali kama za wengine. Unasemaje? Kuhusu njaa, unadhani serikali imeweka juhudi za kutosha kukabili makali ya njaa? Alhamisi serikali ya Kenya ilituma msaada wa chakula Somalia ilhali hapa Kenya watu, mifugo wanaangamia. Kwa mengi wanahabari wetu Collins Chungani akiwa Nyeri, Clinton Ambujo wa Kisumu na Martin Ndiema akiwa Trans Nzoia wameshiriki Gumzo na Wakenya.