Siasa na Gumzo: Jubilee yafufuka? OKA nayo yapata marafiki wapya
Published Feb. 05, 2022
00:00
00:00

Baada ya kimya kingi na fukuzafukuza chamani, hatimaye Rais Uhuru Kenyatta amefanya mkutano na viongozi wa Jubilee katika Ikulu. Ikumbukwe chama hicho kimepanga Mkutano wa Kitaifa wa Wajumbe, NDC tarehe 25 Februari, 2022 katika Ukumbi wa KICC, mjadala ukiwa kuwafurusha rasmi Ruto na wandani wake kutoka chama hicho, mpango wa kushirikiana na miungano mingine na kumfanyia kampeni Raila Odinga. Vilevile mjadala mkali umechacha kuhusu mabadiliko ya Sheria za Uchaguzi. Wana-OKA nao baada ya pigo la kondokewa na Musalia Mudavadi na Moses Wetangula imewapata washirika wengine wawili. Je, ni muungano gani una ufuasi makubwa? Kwa masuala na maswali haya, wanahabari wetu Moses Kiraese wa Pokot Magharibi, Faith Kutere wa Uasin Gishu na Martin Ndiema wa Trans Nzoia wamewashirikisha wakazi katika gumzo wiki hii.