Gumzo la Wiki; Wabunge wa tumbokrasia; si demokrasia wala uwajibikaji
Published Jun. 10, 2022
00:00
00:00

Bunge la 12 limevunjwa rasmi baada ya kuhudumu kwa kipindi cha miaka mitano. Je, limetimiza matarajio ya Wakenya ama limekuwa bunge la demokrasia ama utumbokrasia kwa kujali tu donge nono kupitia marupurupu? Kura za maoni nazo zinaendelea kutolewa kuelekea uchaguzi mkuu. Je, ni za kuaminika ama zinatoa taswira ya kila mwamba ngoma kuvutia kwake? Raila Odinga naye ametangaza manifesto ambayo imeibua gumzo kuu hasa kwa kuzitaja nguo za mitumba kuwa za wafu yaani marehemu. Je, alieleweka visivyo? Wanahabari wetu, Martin Ndiema wa Trans Nzoia, Clintone Ambujo wa Kisumu na Moses Kiraese wa Pokot Magharibi wanatupambia gumzo la wiki hii tukianza na Kiraese.