Gumzo la Wiki Podcast: Raila debeni 2022; Wana'OKA watamuunga nani?
Published Dec. 12, 2021
00:00
00:00

Tangazo la Odinga kuwania urais kwa mara ya tano, ni ithibati kamili kwamba kinyang'anyiro kitakuwa kati yake na William Ruto. Je, hatima ya Kalonzo, Mudavadi na Wetangula ambao walikosa kufika Kasarani ni ipi? Aidha, Wakfu wa Mlima Kenya Foundation, MKFumesema Raila tosha. Je, unadhani wafanyabiashara hao wataamua mwelekeo wa siasa za Mlima Kenya ama ni wananchi ndio watakaoamua jinsi anavyosisitiza William Ruto? Wanahabari wetu, John Mbuthia wa Nyeri, Moses Kiraise wa Pokot Magharibi na Martin Ndiema wa Trans Nzoia wameshiriki gumzo na wakazi wa maeneo yao.