Gumzo la Wiki Podcast; Mudavadi awazuia Odinga na Ruto kuhudhuria NDC
Published Jan. 22, 2022
00:00
00:00

Earthquake aliyoahidi Musalia Mudavadi inasubiriwa kwa hamu kuu Jumapili. Amewaalika wana'OKA na kuwafungia nje Ruto na Raila. Wakenya wana maoni gani? Aidha, cheche baina ya Raila na Ruto zimezidi, kuhusu urushaji mawe na kuitana majina. Haya yanahatarisha utangamano nchini? UDA tayari imeandikia ICC ikidai serikali inafadhili vurugu kwa manufaa ya Raila. Vilevile tunaangazia kesi ya BBI katika Mahakama ya Juu. Je, reggae itarejea? Kadhalika tunazamia suala la mili katika Mto Yala. Wanahabari wetu Moses Kiraese wa Pokot Magharibi, William Omasire wa Nyamira na John Mbuthia wa Nyeri wanatupambia makala haya