Na Mate Tongola
NAIROBI, KENYA, NAIBU Mwalimu mkuu, Walimu watatu, Wanafunzi sita na mzazi wanaendelea kuzuiliwa na maafisa wa polisi kwa kipindi cha siku 10 kwa kuhusishwa na kuteketezwa kwa bweni la shule ya upili ya Karbanet.
Wanafunzi hao na mzazi walikamatwa na kufikishwa mahakamani walikokabiliwa na mashtaka ya uteketezaji kabla ya walimu hao watatu kukamatwa kufuatia maandamano ya wananfunzi na kisha kufunguliwa mashtaka sawa na hayo.
Kwingineko,
Washukiwa wawili akiwamo mwalimu wa Shule ya Upili ya Wasichana ya St.Teresa’s Kaunti ya Trans-Nzoia wameshtakiwa kwa madai ya kupanga kuteketeza shule.
Hata hivyo, hawakuruhusiwa kukana au kubali mashtaka kwa msingi kuwa maafisa wa polisi walihitaji muda zaidi wa kuwachunguza kabla kuwafungulia mashataka.
Wakati uo huo, katika Kaunti ya Kisii ambayo imeathirika zaidi na visa vya uteketezaji wa majengo ya shule, Kamishna wa Kaunti hiyo Kula Hache amepiga marufuku uuzaji wa mafuta ya petroli kwa wanafunzi.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.