Na, Cerel Mulindi/ Beatrice Maganga Ruto azomewa na wananchi Kisumu Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto wameizuru ngome ya mrengo wa NASA, Kaunti ya Kisumu huku msafara wao ukirushiwa mawe na wakazi waliokuwa wakiimba kusifu upinzani. Wawili hao walikuwa aneo hilo kuzindua miradi kadhaa ya maendeleo vilevile kuendeleza kampeni za kisiasa. Wakihutubu katika eneo la Ahero ambako Rais alizindua mradi wa kukarabati barabara kuu ya Ahero- Kisii, Rais Kenyatta ameisifu serikali ya Jubilee kwa baadhi ya miradi ambayo imewatekelezea wananchi. Naibu wake, William Ruto aidha amesema serekali imejitolea kusambaza umeme nchini huku idadi ya walionufaika eneo hili ikiongozeka kutoka elfu 40 mwaka wa 2013 hadi elfu190, mradi ambao umegharimu kima cha shilingi bilioni 1.2. Kwenye eneo la Okore ambako Rais amezindua mradi wa Kampuni ya East African Breweries wa ujenzi wa kiwanda cha pombe kwa kuweka jiwe la msingi, wakazi wamemzomea Naibu wake, William Ruto huku wakimzuia kuhutubia umma. Juhudi za Ruto kuwatuliza wakazi ziliambulia patupu na kumlazimu Rais kuingilia kati. Rais Kenyatta amesema ujenzi wa kiwanda hicho utachangia pakubwa ukuzaji wa uchumi wa taifa hili vilevile kubuni nafasi zaidi za ajira kwa wakazi. Rais aidha amezindua ujenzi wa kituo cha kupakia mafuta katika Ziwa Victoria ambacho amesema kitaanza kutumika kufikia mwezi Okotoba. Awali Rais amezindua rasmi Kivukio cha Mbita kwenye Kaunti ya Homabay kilichogharimu shilingi bilioni 1.5. Ujenzi wa kivukio hicho ulianza baada ya watu kadhaa kuaga dunia kwa kujaribu kuvuka Ziwa Victoria baina ya visiwa vya Rusinga na Mbita. Wawili hao aidha wamewarai wakazi kuwapigia kura wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Ruto azomewa na wananchi Kisumu
Living
By | 8 years ago | 2 Min read
.
Trending Now
- Signs you're ready for entrepreneurship
- Brace for higher fuel prices over three years as regulator digs in
- Can an extrovert and introvert really make love work?
- Mum with 'blocked nose' to lose sight and teeth in cancer fight
- Beauty on a budget: Looking your best without overspending
- Is it possible to stay friends with your ex?
- Watch out for these sweet flavours that could kill you
- Host a fabulous festive season without overspending
- Girls' night out has a lot more than you imagine
- Reeney Music: Kenyan food reminds me of my roots
.
Popular this week
- Love, duty and exhaustion: Silent strain of supporting ageing parents
- Why does everything always go wrong for me?
- Beauty on a budget: Looking your best without overspending
- I got intimate with my step-dad and it's killing me
- I don't want to get sexually active with my new boyfriend
- Easy recipe: Crispy calamari
- Jobs that cause impotence among Kenyan men
- Five benefits of bikini waxing
- Recipe: Hybrid biriani
- Kim Kardashian spotted without wedding ring as she heads out before Valentine's Day
.
Similar Articles
.
Latest Articles
Living
By Jael Wakesho
Jun. 6, 2026
Between The Sheets
Jun. 6, 2026
.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.