Na, Cerel Mulindi/ Beatrice Maganga Ruto azomewa na wananchi Kisumu Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto wameizuru ngome ya mrengo wa NASA, Kaunti ya Kisumu huku msafara wao ukirushiwa mawe na wakazi waliokuwa wakiimba kusifu upinzani. Wawili hao walikuwa aneo hilo kuzindua miradi kadhaa ya maendeleo vilevile kuendeleza kampeni za kisiasa. Wakihutubu katika eneo la Ahero ambako Rais alizindua mradi wa kukarabati barabara kuu ya Ahero- Kisii, Rais Kenyatta ameisifu serikali ya Jubilee kwa baadhi ya miradi ambayo imewatekelezea wananchi. Naibu wake, William Ruto aidha amesema serekali imejitolea kusambaza umeme nchini huku idadi ya walionufaika eneo hili ikiongozeka kutoka elfu 40 mwaka wa 2013 hadi elfu190, mradi ambao umegharimu kima cha shilingi bilioni 1.2. Kwenye eneo la Okore ambako Rais amezindua mradi wa Kampuni ya East African Breweries wa ujenzi wa kiwanda cha pombe kwa kuweka jiwe la msingi, wakazi wamemzomea Naibu wake, William Ruto huku wakimzuia kuhutubia umma. Juhudi za Ruto kuwatuliza wakazi ziliambulia patupu na kumlazimu Rais kuingilia kati. Rais Kenyatta amesema ujenzi wa kiwanda hicho utachangia pakubwa ukuzaji wa uchumi wa taifa hili vilevile kubuni nafasi zaidi za ajira kwa wakazi. Rais aidha amezindua ujenzi wa kituo cha kupakia mafuta katika Ziwa Victoria ambacho amesema kitaanza kutumika kufikia mwezi Okotoba. Awali Rais amezindua rasmi Kivukio cha Mbita kwenye Kaunti ya Homabay kilichogharimu shilingi bilioni 1.5. Ujenzi wa kivukio hicho ulianza baada ya watu kadhaa kuaga dunia kwa kujaribu kuvuka Ziwa Victoria baina ya visiwa vya Rusinga na Mbita. Wawili hao aidha wamewarai wakazi kuwapigia kura wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Ruto azomewa na wananchi Kisumu
Living
By | 8 years ago | 2 Min read
.
Trending Now
- 'Yellow wave' sweeps political also-rans in Mt Kenya to power
- Hepatitis C-HIV co-infection higher among drug injectors
- Mudavadi role as Prime Cabinet Secretary
- According to research, full time work may be bad for your brain
- Soft launching love: Privacy, protection or a red flag?
- Benefits of using rose water on your skin
- Reasons you feel sleepy in the afternoon
- How to use your silverware and dinner ware
- The importance of keeping a journal
- 10 health benefits of eating bananas during pregnancy
.
Popular this week
- How perfectionism starts in childhood
- 10 health benefits of eating bananas during pregnancy
- Keeping passion alive after 'I Do'
- The importance of keeping a journal
- Three ways you can easily find love
- Soft launching love: Privacy, protection or a red flag?
- Five factors to consider before dyeing your hair
- Drowning in debt? Here's how to break free
- How to wear bold prints with confidence
- Food of the week: Honey
.
Similar Articles
.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.