Na, Cerel Mulindi/ Beatrice Maganga Ruto azomewa na wananchi Kisumu Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto wameizuru ngome ya mrengo wa NASA, Kaunti ya Kisumu huku msafara wao ukirushiwa mawe na wakazi waliokuwa wakiimba kusifu upinzani. Wawili hao walikuwa aneo hilo kuzindua miradi kadhaa ya maendeleo vilevile kuendeleza kampeni za kisiasa. Wakihutubu katika eneo la Ahero ambako Rais alizindua mradi wa kukarabati barabara kuu ya Ahero- Kisii, Rais Kenyatta ameisifu serikali ya Jubilee kwa baadhi ya miradi ambayo imewatekelezea wananchi. Naibu wake, William Ruto aidha amesema serekali imejitolea kusambaza umeme nchini huku idadi ya walionufaika eneo hili ikiongozeka kutoka elfu 40 mwaka wa 2013 hadi elfu190, mradi ambao umegharimu kima cha shilingi bilioni 1.2. Kwenye eneo la Okore ambako Rais amezindua mradi wa Kampuni ya East African Breweries wa ujenzi wa kiwanda cha pombe kwa kuweka jiwe la msingi, wakazi wamemzomea Naibu wake, William Ruto huku wakimzuia kuhutubia umma. Juhudi za Ruto kuwatuliza wakazi ziliambulia patupu na kumlazimu Rais kuingilia kati. Rais Kenyatta amesema ujenzi wa kiwanda hicho utachangia pakubwa ukuzaji wa uchumi wa taifa hili vilevile kubuni nafasi zaidi za ajira kwa wakazi. Rais aidha amezindua ujenzi wa kituo cha kupakia mafuta katika Ziwa Victoria ambacho amesema kitaanza kutumika kufikia mwezi Okotoba. Awali Rais amezindua rasmi Kivukio cha Mbita kwenye Kaunti ya Homabay kilichogharimu shilingi bilioni 1.5. Ujenzi wa kivukio hicho ulianza baada ya watu kadhaa kuaga dunia kwa kujaribu kuvuka Ziwa Victoria baina ya visiwa vya Rusinga na Mbita. Wawili hao aidha wamewarai wakazi kuwapigia kura wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Ruto azomewa na wananchi Kisumu
Living
By | 8 years ago | 2 Min read
.
Trending Now
- Drowning in debt? Here's how to break free
- Why the average wedding in Kenya costs 3.5 Million and could go higher
- Why mums should let their children know their father
- A big salute to all of you working hard at being good fathers
- How perfectionism starts in childhood
- Arimis is bae: Why milking jelly is the new cosmetic craze among women
- Just how much do women spend on makeup?
- What happens when the Queen dies?
- UN urges action on cryptocurrencies in developing states
- Would YOU know how to save your child's life? Follow our top tips to make sure you do
.
Popular this week
- How perfectionism starts in childhood
- Soft launching love: Privacy, protection or a red flag?
- Drowning in debt? Here's how to break free
- From tout to CEO
- Kenyatta akutana na Ruto katika Ikulu
- Dad with one week to live sets up heartbreaking fundraising page for wife and daughter
- A big salute to all of you working hard at being good fathers
- Health chatbots can be useful, but they should not substitute a doctor
- Why you need a partner in life
- Two boys left to die as parents prayed after circumcision ceremony goes awry
.
Similar Articles
.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.