Na, Cerel Mulindi/ Beatrice Maganga Ruto azomewa na wananchi Kisumu Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto wameizuru ngome ya mrengo wa NASA, Kaunti ya Kisumu huku msafara wao ukirushiwa mawe na wakazi waliokuwa wakiimba kusifu upinzani. Wawili hao walikuwa aneo hilo kuzindua miradi kadhaa ya maendeleo vilevile kuendeleza kampeni za kisiasa. Wakihutubu katika eneo la Ahero ambako Rais alizindua mradi wa kukarabati barabara kuu ya Ahero- Kisii, Rais Kenyatta ameisifu serikali ya Jubilee kwa baadhi ya miradi ambayo imewatekelezea wananchi. Naibu wake, William Ruto aidha amesema serekali imejitolea kusambaza umeme nchini huku idadi ya walionufaika eneo hili ikiongozeka kutoka elfu 40 mwaka wa 2013 hadi elfu190, mradi ambao umegharimu kima cha shilingi bilioni 1.2. Kwenye eneo la Okore ambako Rais amezindua mradi wa Kampuni ya East African Breweries wa ujenzi wa kiwanda cha pombe kwa kuweka jiwe la msingi, wakazi wamemzomea Naibu wake, William Ruto huku wakimzuia kuhutubia umma. Juhudi za Ruto kuwatuliza wakazi ziliambulia patupu na kumlazimu Rais kuingilia kati. Rais Kenyatta amesema ujenzi wa kiwanda hicho utachangia pakubwa ukuzaji wa uchumi wa taifa hili vilevile kubuni nafasi zaidi za ajira kwa wakazi. Rais aidha amezindua ujenzi wa kituo cha kupakia mafuta katika Ziwa Victoria ambacho amesema kitaanza kutumika kufikia mwezi Okotoba. Awali Rais amezindua rasmi Kivukio cha Mbita kwenye Kaunti ya Homabay kilichogharimu shilingi bilioni 1.5. Ujenzi wa kivukio hicho ulianza baada ya watu kadhaa kuaga dunia kwa kujaribu kuvuka Ziwa Victoria baina ya visiwa vya Rusinga na Mbita. Wawili hao aidha wamewarai wakazi kuwapigia kura wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Ruto azomewa na wananchi Kisumu
Living
By | 8 years ago | 2 Min read
.
Trending Now
- When hosting a relative, lay down the rules
- Delicate dance: What reciprocity really looks like in relationships
- Don’t forget me yet-Daddy Owen speaks out!!
- Too broke to shoot a film? Relax, I will sort you out
- How to burn calories through walking
- Ingredient of the week: Aliya (Beef jerky)
- How you can stay safe when clubbing
- How to work from home with the kids around
- It was one to forget: Michelle was angry at Obama for bringing her to Kenya
- Scuffle as Raila Odinga's bodyguard blocked from Nyayo VIP lounge
.
Popular this week
- Elevate your graphic T-shirt into a fashion statement
- Easy recipe: Muhogo wa nazi
- Easy recipe: Char-grilled chicken tikka
- Red flags you should watch out for before getting married
- Too broke to shoot a film? Relax, I will sort you out
- Slain rapper Takeoff to be remembered at Atlanta celebration
- Do you know your woman's love language?
- Bloated? Here are the top common causes
- Why does wanting more make me difficult?
- How to get rid of enlarged pores
.
Similar Articles
.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.