Na, Cerel Mulindi/ Beatrice Maganga Ruto azomewa na wananchi Kisumu Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto wameizuru ngome ya mrengo wa NASA, Kaunti ya Kisumu huku msafara wao ukirushiwa mawe na wakazi waliokuwa wakiimba kusifu upinzani. Wawili hao walikuwa aneo hilo kuzindua miradi kadhaa ya maendeleo vilevile kuendeleza kampeni za kisiasa. Wakihutubu katika eneo la Ahero ambako Rais alizindua mradi wa kukarabati barabara kuu ya Ahero- Kisii, Rais Kenyatta ameisifu serikali ya Jubilee kwa baadhi ya miradi ambayo imewatekelezea wananchi. Naibu wake, William Ruto aidha amesema serekali imejitolea kusambaza umeme nchini huku idadi ya walionufaika eneo hili ikiongozeka kutoka elfu 40 mwaka wa 2013 hadi elfu190, mradi ambao umegharimu kima cha shilingi bilioni 1.2. Kwenye eneo la Okore ambako Rais amezindua mradi wa Kampuni ya East African Breweries wa ujenzi wa kiwanda cha pombe kwa kuweka jiwe la msingi, wakazi wamemzomea Naibu wake, William Ruto huku wakimzuia kuhutubia umma. Juhudi za Ruto kuwatuliza wakazi ziliambulia patupu na kumlazimu Rais kuingilia kati. Rais Kenyatta amesema ujenzi wa kiwanda hicho utachangia pakubwa ukuzaji wa uchumi wa taifa hili vilevile kubuni nafasi zaidi za ajira kwa wakazi. Rais aidha amezindua ujenzi wa kituo cha kupakia mafuta katika Ziwa Victoria ambacho amesema kitaanza kutumika kufikia mwezi Okotoba. Awali Rais amezindua rasmi Kivukio cha Mbita kwenye Kaunti ya Homabay kilichogharimu shilingi bilioni 1.5. Ujenzi wa kivukio hicho ulianza baada ya watu kadhaa kuaga dunia kwa kujaribu kuvuka Ziwa Victoria baina ya visiwa vya Rusinga na Mbita. Wawili hao aidha wamewarai wakazi kuwapigia kura wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Ruto azomewa na wananchi Kisumu
Living
By | 8 years ago | 2 Min read
.
Trending Now
- Touching: Gospel singer Esther Wahome opens up on challenges of raising an autistic son
- Unlock the true power of your mind
- Health chatbots can help but they shouldn't replace your doctor
- Taking off: My journey into luxury fashion
- Benefits of getting laid during pregnancy
- Watch out! How rhesus factor affects your unborn child
- I can't seem to make relationships work
- Things you should know before dating a single mum
- Is 50 the new 20? Meet Arnita Champion the 54-year-old hottie
- Mwilu rejects claim that Judiciary is in bed with the State
.
Popular this week
- C-Section Awareness Month: Stories behind the scar
- 4 things you should be eating to get a healthy glow
- Thinking of resigning? Here's how to do it right
- Is choreromance the future of dating?
- How to wear stripes like a fashion pro
- Dreaming your partner is cheating on you? This and other common dreams explained by expert
- Return of 'analogue hobbies' in a digital age
- Bad boy: Why women don’t bring their men gifts when they travel
- Simple car seat trick that takes two minutes but could save a child's life
- Why you should always re-heat rice with a wet towel over the bowl
.
Similar Articles
.
Latest Articles
.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.