Na, Cerel Mulindi/ Beatrice Maganga Ruto azomewa na wananchi Kisumu Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake, William Ruto wameizuru ngome ya mrengo wa NASA, Kaunti ya Kisumu huku msafara wao ukirushiwa mawe na wakazi waliokuwa wakiimba kusifu upinzani. Wawili hao walikuwa aneo hilo kuzindua miradi kadhaa ya maendeleo vilevile kuendeleza kampeni za kisiasa. Wakihutubu katika eneo la Ahero ambako Rais alizindua mradi wa kukarabati barabara kuu ya Ahero- Kisii, Rais Kenyatta ameisifu serikali ya Jubilee kwa baadhi ya miradi ambayo imewatekelezea wananchi. Naibu wake, William Ruto aidha amesema serekali imejitolea kusambaza umeme nchini huku idadi ya walionufaika eneo hili ikiongozeka kutoka elfu 40 mwaka wa 2013 hadi elfu190, mradi ambao umegharimu kima cha shilingi bilioni 1.2. Kwenye eneo la Okore ambako Rais amezindua mradi wa Kampuni ya East African Breweries wa ujenzi wa kiwanda cha pombe kwa kuweka jiwe la msingi, wakazi wamemzomea Naibu wake, William Ruto huku wakimzuia kuhutubia umma. Juhudi za Ruto kuwatuliza wakazi ziliambulia patupu na kumlazimu Rais kuingilia kati. Rais Kenyatta amesema ujenzi wa kiwanda hicho utachangia pakubwa ukuzaji wa uchumi wa taifa hili vilevile kubuni nafasi zaidi za ajira kwa wakazi. Rais aidha amezindua ujenzi wa kituo cha kupakia mafuta katika Ziwa Victoria ambacho amesema kitaanza kutumika kufikia mwezi Okotoba. Awali Rais amezindua rasmi Kivukio cha Mbita kwenye Kaunti ya Homabay kilichogharimu shilingi bilioni 1.5. Ujenzi wa kivukio hicho ulianza baada ya watu kadhaa kuaga dunia kwa kujaribu kuvuka Ziwa Victoria baina ya visiwa vya Rusinga na Mbita. Wawili hao aidha wamewarai wakazi kuwapigia kura wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Ruto azomewa na wananchi Kisumu
Living
By | 8 years ago | 2 Min read
.
Trending Now
- Need a man? Here's how to get one in 2018
- Woman disgusted after racist date told her she didn’t ‘smell like black people’
- Grim future for local firms as venture capital gravy train slows
- Does you baby have dry skin? Here are 6 ways to take care of a baby's dry skin
- Is celebrated gospel artist Mary Atieno facing domestic negligence from her husband?
- Netizens go wild over Lionel Richie’s much younger girlfriend
- Senate starts formal process to kick out four IEBC commissioners
- Wearing makeup on sensitive skin
- Photos: A look into Maureen Waititu's beautiful home
- Shade Systems entrepreneur Eric Kinoti;I make millions but I'm not a millionaire...yet
.
Popular this week
- Wearing makeup on sensitive skin
- December done right: Enjoy the festive season without burning out
- Your child is a reservoir of respiratory bugs, learn how to minimise harm
- Cocktail bar: Lemongrass gimlet
- The smartphone has transformed life for better and for worse
- Gentlemen, these are the mistakes you make when going for ‘ruracio’
- Why can't celebrity relationships last?
- Should men be taught how to love?
- How to cut travel costs and still have fun
- "Gossip Girl" star Leighton Meester to join husband Adam Brody on Season 2 of 'Nobody Wants This'
.
Similar Articles
.
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media
platforms spanning newspaper print
operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a
leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national
and international interest.