Ama kwa hakika waliosema kuwa “pesa zilivunja mlima”, kweli hawakuwa na mzaha wa maana hiyo. Na tamaa nayo, pia wahenga walisema ilimpasua “fisi” msamba!
Mfanyabiashara anayedai kuwa mlalamishi wa kesi iliyomtorosha Gavana wa Nairobi Mike Sonko Mbuvi kutoka jela ya Shimo la Tewa mnamo mwaka 1998, amerejea tena mahakama kuu ya Mombasa kuwasilisha kesi mpya kudai alipwe zaidi ya shilingi milioni 10 anazodai kulaghaiwa miaka 21 iliyopita.