Idara ya Upelelezi DCI imeanzisha uchunguzi kufuatia madai ya ulaghai wa mpango wa masomo kwa wanafunzi kutoka Kaunti ya Uasin Gishu waliofaa kusomea nchini Finland na Canada.
Katika taarifa yake jioni hii DCI imesema hatua hiyo inafuatia malalamiko kutoka kwa wakazi wanaodai kulaghaiwa mamilioni ya pesa wakiahidiwa kuwa wanao wangefadhiliwa kusomea nchini humo.
Maafisa wa DCI wanatarajiwa kuelekea Uasin Gishu kati ya Julai 18 hadi tarehe 21 kuendeleza uchunguzi zaidi.
Waathiriwa wote wameshauriwa kujiwasilisha katika makao makuu ya DCI mjini Eldoret kurekodi taarifa.