×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Ruto aahidi serikali yake itazingatia haki

Living

Rais Mteule, William Ruto amewahakikishia Wakenya kwamba serikali yake itazingatia haki kwa kila mmoja na kudumisha demokrasia katika utendakazi wake bila mwingilio wa taasisi za serikali.

Akiwahutubia viongozi wa Muungano wa Kenya Kwanza mtaani Karen hapa Nairobi, Ruto amesisitiza kwamba serikali yake itazingatia sheria na kuheshimu katiba.

Katika kikao hicho, Ruto aidha amewahimiza viongozi hao kujiandaa vilivyo kutekeleza ahadi walizoweka wakati wa kampeni akisema wana jukumu kubwa la kufanikisha miradi ya maendeleo mashinani.

Wakati uo huo, Ruto amewaomba viongozi wote nchini kushirikiana na serikali yake, ili kuwahudumia Wakenya waliowachagua.

Vilevile Ruto amewahakikishia Wakenya kwamba serikali yake itawajibikia maslahi yao kwa hali yoyote ile. Katika kufanikisha hilo, Ruto amesema kupitia uongozi wa mabunge la Kitaifa na Seneti yatapitisha mswada unaolenga kuwashurutisha mawaziri kufika mbele ya bunge kujibu maswali kuhusu utendakazi wa wizara zao. Aidha, ameongeza kwamba serikali yake haitakubali watumishi wa umma kujihusisha na siasa.

Katika Muungano wa Kenya Kwanza mia moja sitini na watatu ambapo wa Chama cha UDA kina mia moja arubaini na maseneta ishirini na wanne. Aidha wabunge huru kumi miongoni mwa kumi na wawili waliochaguliwa majuzi vilevile wamejiunga na Kenya Kwanza.

Related Topics


.

Similar Articles

.

Recommended Articles