×
App Icon
The Standard e-Paper
Truth Without Fear
★★★★ - on Play Store
Download Now

Raila asema Afrika imelalia masikio utajiri wake

Aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga akihutubia watu katika hafla ya kuzindua kitabu jijini Kisumu. [Picha: Standard]

Asasi sufufu za kimataifa hususan za kifedha zimethibitisha kuwa Afrika ni sehemu pekee duniani ambayo ina raslimali za kiuchumi kushinda sehemu nyingine. “Simba wa Afrika anamwambia simba marara (Tiger) wa Asia kwamba nimekalia mali na nakuja kutawala,” asema kimafumbo Raila Odinga katika hotuba yake ya umoja wa wafanyikazi Afrika jijini Nairobi majuzi. Raila anamini kuwa Afrika ina uwezo wa kuwa mbele kimaendeleo kushinda mabara mengine kama Ulaya na Amerika. Swali ni, Je, kuwaje Afrika iliyo tajiri kuwa kama masikini anayeomba misaada kwa ‘matajiri’ wa nje?

Je, ni sababu zipi za kinaya hiki cha Afrika na suluhu iko wapi? Sambamba na imani ya Raila aliye mjumbe maalum wa miundo mbinu katika Umoja wa Afrika (AU) ni kweli Afrika imelalia masikio. Penye miti hakuna wajenzi. Msemo huu ndio ukweli uliopo kwa bara la Afrika na ni changamoto kubwa katika karne hii ya utandawazi inayotowa fursa ya kuendelea badala ya kuzembea.

Get Full Access for Ksh299/Week
Unlock the Full Story — Join Thousands of Informed Kenyans Today
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in