Raila asema Afrika imelalia masikio utajiri wake

Aliyekuwa waziri mkuu Raila Odinga akihutubia watu katika hafla ya kuzindua kitabu jijini Kisumu. [Picha: Standard]

Asasi sufufu za kimataifa hususan za kifedha zimethibitisha kuwa Afrika ni sehemu pekee duniani ambayo ina raslimali za kiuchumi kushinda sehemu nyingine. “Simba wa Afrika anamwambia simba marara (Tiger) wa Asia kwamba nimekalia mali na nakuja kutawala,” asema kimafumbo Raila Odinga katika hotuba yake ya umoja wa wafanyikazi Afrika jijini Nairobi majuzi. Raila anamini kuwa Afrika ina uwezo wa kuwa mbele kimaendeleo kushinda mabara mengine kama Ulaya na Amerika. Swali ni, Je, kuwaje Afrika iliyo tajiri kuwa kama masikini anayeomba misaada kwa ‘matajiri’ wa nje?

Je, ni sababu zipi za kinaya hiki cha Afrika na suluhu iko wapi? Sambamba na imani ya Raila aliye mjumbe maalum wa miundo mbinu katika Umoja wa Afrika (AU) ni kweli Afrika imelalia masikio. Penye miti hakuna wajenzi. Msemo huu ndio ukweli uliopo kwa bara la Afrika na ni changamoto kubwa katika karne hii ya utandawazi inayotowa fursa ya kuendelea badala ya kuzembea.

Utajiri wa Afrika umetapakaa lakini haujatumiwa vilivyo mfano wa ng’ombe aliyejaa maziwa na kukosa mkamuaji wa kutowa maziwa hayo. Afrika ina madini sufufu, bahari kubwa, mito, maziwa , ardhi ya rotuba, gesi, mafuta na mazao mbali mbali ya kilimo.Kinaya ni kuwa nchi nyingi za Afrika hutegemea misaada hata ya chakula kutoka nje ya bara. Afria ina uwezo wa kulisha ulimwengu mzima lakini sasa inalishwa na mataifa ya nje.Je, tatizo liko wapi na suluhu ni ipi? Ukoloni mkongwe na ukoloni mambo leo ndio chanzo cha kukoro? sha tunu ya utajiri wa Afrika.Utumwa huu ndio adui mkubwa wa Afrika. Ukoloni mkongwe ulitowa fursa kwa wazungu kupora na ziada ya yote kudhibiti raslimali za Afrika.Walikuja na mpango makhususi wa kusimamia nyanzo zote za uchumi.

Makampuni makubwa ya wazungu yalitawala uchumi wa Afrika huku yakilindwa na serikali zao mama waliokuwa na nguvu za mtutu wa bunduki. Kampuni kama Cadbury Chocklate walidhibiti mashamba ya cocoa kule Afrika magharibi na kusa? risha milima ya zao hilo na kutengeneza ulaya bidhaa hiyo na kuuza tena kwa wafrika. Kampuni ya zao la mipira la Firestone pia ilipora zao la mipira yaani rubber kutoka Afrika na kutengeneza magurudumu ya magari na kuza kwa faida. Kimsingi wafrika haakupata fursa ya kuwa na makampuni ya kutengeneza malighasi zao ambapo wazungu walipora na kutengeneza kule ulaya.

Siri kuu ni Afrika kuzinduka na kuboreha raslimali zao bila msaada wa m? sadi mzungu na mporaji.Hii inaezekana kukiwa na mikakati ya kuwa na watalamu wa sekta ya utengezaji na uundaji. Umoja wa Afrika ndio nguvu thabiti za kudhibiti hujuma za uporaji wa waziungu dhidi ya bara hili.Ni sharti Arika kukoma kutegemea wazungu kiuchumi. Tukumbuke msukumo wa ukoloni ulikuwa kupata masoko na raslimali toka Afrika kufaidi wakoloni na watu wao. Sambamba na wazo la Raila ni muhimu kuiga mfano wa Uchina ambayo inategemea watu wake kama wafanyikazi na wanunuzi wa bidhaa zao. Habari njema ni kuwa Afrika imeweza kugundua kasoro hizi na sasa inaamka kama simba alonyeshewa na aliyekuwa amelala na kutishia utawala wa simba marara.