Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Home To Bold Columnists
★★★★ - on Play Store
Download App

Ukumbusho wa Kijana Wamalwa wafanyika

Na, Martin Ndiema
Ukumbusho wa Kijana Wamalwa wafanyika
Maadhimisho ya 14 tangu kufariki dunia kwa aliyekuwa Makamu wa Rais, Kijana Wamalwa yamefanyila leo hii nyumbani kwake mjini Kitale Kaunti ya Trans Nzoia huku suala kuhusu uchaguzi mkuu uliokamilika likishamiri. Aidha viongozi wengine waliohutubu halfa hiyo wameyakosoa matamshi yanayotolewa kuhusu uwezekano wa kuligawanya taifa kwa misingi ya miegemeo ya kisiasa.
Akihutubu wakati wa hafla hiyo, kakaye marehemu ambaye ni Waziri wa Maji, Eugene Wamalwa amewapongeza wakazi wa eneo la Magharibi ya Nchi kwa kuwahakikishia ushindi baadhi ya wanasiasa waliowania viti vya uongozi kupitia Chama cha Jubilee.
Aidha kauli ya Mwanauchumi na Mchanganuzi wa Masuala ya Kisiasa, David Ndii ya kuunga mkono kugawanywa kwa taifa hili kwa misingi ya kisiasa, imeibua hisia miongoni mwa viongozi waliohudhuria ibada hiyo. Mbunge mteule wa Kimilili, Ditmus Barasa na mwenzake wa Endebess, Daktari Robert Pukose wamewarai maafisa wa usalama kumchukulia Ndii hatua kali za kisheria.  Kauli ya viongozi hao imetiliwa mkazo na Mbunge mteule wa Sirisia John Waluke.  
Si hayo tu, aliyekuwa Mbunge wa Matungu David Were na mwenzake wa Saboti, David Lazarus wamewashauri Wakenya kudumisha amani.
Kijana Wamalwa alikuwa Makamu wa Rais wakati wa utawaka wa Rais Mstaafu, Mwai Kibaki na alifariki dunia mwaka 2003 baada ya kuhudumu katika wadhifa huo kwa kipindi cha miezi minane.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Related Topics