Eliot Berry, Mwingereza anayependelea kuishi Kenya| Kisa Changu Podcast
Published Nov. 27, 2022
00:00
00:00

Eliot Berry, Raia wa Uingereza alikuja Kenya akiwa na umri wa miaka 19 alipotumwa na mamaye kutembea. Anasema alikuwa msumbufu na mara nyingi alikuwa akitoroka shuleni lakini alipofika Kenya alihisi kuwa nyumbani na maisha yake yakabadilika. Alianza rasmi kuishi nchini Kenya mwaka 2011 na amejifunza Kiswahili na pia Sheng kwa lengo la kutangamana na watu wa matabaka yote. Aidha, kwenye mitandao ya kijamii anakojulikana kama Reverend Dad, amekuwa akiwafurahisha watu kwa video za ucheshi kutumia Kiswahili. Katika Kicha Changu Podcast wiki hii tunaangazia maisha ya Reverend Dad, katika mahojaino haya na Faith Kutere.