IEBC yawafuta maafisa 4 Homa Bay

Tume ya Uchaguzi, IEBC imewafuta kazi maafisa wake 4 ambao walikamatwa katika Eneo Bunge la Ndhiwa kwenye Kaunti ya Homa Bay wakihusishwa na njama za kulenga kufanikishwa udanganyifu katika uchaguzi wa Jumanne wiki hii.

Waliofutwa ni msimamizi wa uchaguzi katika kituo kimoja cha kupigia kura katika wadi ya Kanyadoto, manaibu wasimamizi wa uchaguzi wa vituo viwili vya kupigia kura katika wadi ya Kanyadoto na karani wa kituo kimoja cha wadi ya Kwabwai.

Wanne hao walifumaniwa na wananchi wakiwa katika kikao na baadhi ya wagombea wa chama kimoja cha kisiasa kwenye eneo hilo katika kijiji cha Riat.

IEBC inatarajiwa kuwaajiri wengine wapya kuchukua nafasi yao.