Wandani wa mgombea wa urais wa Chama cha Azimio, Raila Odinga wameendeleza shutuma zao dhidi ya mshinadni wao William Ruto wa UDA, na kumtaja kuwa kiongozi mwenye hasira hivyo basi hafai kuongoza taifa.
Akizungumza wakati wa misururu ya kampeni za kumtafutia Odinga kura hapa Jijini Nairobi, Kingozi wa WIPER Kalonzo Musyoka na Mwenyekiti wa Kamati ya Kampeni za Odinga, Gavana Laikipia Nderitu Mureithi wamemtaja Ruto na wandani wake kuwa wanafiki wanaondelea kuonesha hasira zao wazi licha ya kumshtumu Rias Kenyatta kwamba anamshambulia visivyo.