Watu wamethibitishwa kufariki dunia kufuatia ajali iliyoyahusisha magari kadhaa katika eneo la Kosachei Barabara Kuu ya Eldoret-Webuye.
Inasemekana ajali hiyo iliyahusisha malori mawili na magari mawili ya abiria.
Mkuu wa Polisi wa Uasin Gishu Ayub Gitonga amesema gari moja ya abiria iligongana na lori lililokuwa likielekea Webuye.
Dakika chache baadaye gari jingine lililokuwa likielekea Eldoret lilisimama katika eneo la ajali na hapo ndipo liligongw ana lori lililokuwa likiendeshwa kwa kasi kuelekea Eldoret.
Gitonga amesema lori hilo liliisukuma gari na kusababisha ianguke. Majeruhi kumi wa ajali hiyo wamepelekwa hospitali kwa matibabu.