Gavana wa Kajiado Dkt David Nkedianye amemsuta mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria na kumtaja kama asiye na maadili yanawafaa viongozi wenye nembo ya ‘mheshimiwa’.
Akizungumza kwenye mahojiano Jumatano asubuhi katika Radio Maisha, Nkedianye amesema kwa wakati mmoja mbunge huyo alitusi viongozi katika eneo la Isinya na kumtaka akome tabia hiyo.