Idara ya Utabiri wa Hali ya Anga, imetoa wito kwa Wakazi wa Kaunti za Mombasa, Kilifi, Lamu, Kwale na Tana River kuwa makini kwani mvua kubwa inatarajiwa kunyesha maeneo hayo kuanzia leo.
Mvua hiyo kubwa yenye waviwango vya milimita 20, inatarajiwa kushuhudiwa leo huku viwango hivyo vikiongezeka hadi milimita 40 kufikia tarehe saba. Aidha itapungua tarehe nane huku ikiambatana na upepo mkali.
Mshirikishi wa Shirika la Msalaba Mwekundu tawi la Kwale Mohammed Mwaenzi, ametoa wito kwa wakazi wa Vanga, Kiwegu, Jasini na Jego kuwa wangaalifu wakati huu, vilevile akiwatahadharisha watu wanaozuru fuo za bahari sawa na wavuvi kuwa wangalifu, kwani mvua hiyo inatarajiwa kuambatana na upepo mkali.
Hata hivyo, amesema kwamba Shirika hilo limejiandaa kukabiliana na majanga yoyote ambayo yatasababishwa na mvua hiyo.