Pigo kwa ODM baada Jopo la Kutatua Mizozo ya Vyama vya Kisiasa kuongeza muda wa kumtimua jumwa

Jopo la Kutatua Mizozo ya Vyama vya Kisiasa limeongeza muda wa kuzuia Chama cha ODM kumtimua kabisa Mbunge wa Malindi Aisha Jumwa na kukipa chama hicho siku 10 kuwasialiana na jopo hilo.

Akihutubu mapema leo katika Soko la Toi, kwenye Mtaa wa Kibera,  Kinara wa chama hicho, Raila Odinga alisema Jumwa anaweza kurejeshwa kuwa mwanachama wa ODM iwapo ataomba msamaha.

Kauli ya Raila ilijiri siku mbili tu baada ya viongozi wanawake wa chama hicho kumtaka Jumwa kumheshimu Raila na kukoma kumhusisha na masaibu yake, hasa baada ya Baraza Kuu la Chama hicho kuidhinisha pendekezo la kumtimua chamani.

Wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa ODM, Agnes Zani, walisema Jumwa alijisababishia masaibu hayo baada ya kukiuka katiba ya chama, ambapo uamuzi wa kuondolewa kwake uliafikiwa na wanachama wote.

Related Topics

aisha jumwa