Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Kenya’s Boldest Voice
★★★★ - on Play Store
Download App

IEBC yawataka wabunge kupitisha bajeti


Na Beatrice Maganga
NAIROBI, KENYA, Ikiwa imesailia miezi michache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu, Tume ya Uchaguzi, IEBC imetoa wito kwa bunge kusuluhisha suala la bajeti ya tume hiyo haraka iwezekanavyo.
Afisa Mkuu Mtendaji wa tume hiyo, Ezra Chiloba amesema licha ya tume kuwasilisha makadirio yake ya kima cha shilingi bilioni 31 ya kuandaa uchaguzi huo, bunge halijawasiliana na tume hiyo kuhusu mapendekezo yake.
Chiloba amesema kufikia sasa IEBC imepokea shilingi bilioni 19 pekee. Hata hivyo ameeleza matumaini kwamba  zilizosalia zitatolewa kwa wakati.
Wakati uo huo, amesema IEBC imeanza upya shughuli ya kutoa kandarasi za uchapishaji karatasi za kura baada ya mahakama kufutilia mbali tenda iliyopewa kampuni ya Al Ghurair ya Dubai.
Chiloba alikuwa akizungumza wakati wa warsha ya makamishna wa tume iliyoandaliwa katika hoteli moja mjini Niavasha. Warsha hiyo ilihudhuriwa na maafisa wengine wa uchaguzi kutoka mataifa ya Afrika Kusini, Namibia, Nigeria na Ghana.

 

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Fact-first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News

Related Topics

IEBC Ezra Chiloba