Isaack Lenaola ateuliwa kuwa jaji katika mahakama ya juu

Na Mike Nyagwoka

Jina la Jaji wa Mahakama Kuu, Isaac Lenaola linatarajiwa kuwasilishwa kwa Rais ili kuanza mchakato wa kumwidhinisha kuwa Jaji wa Mahakama ya Juu. Lenaola ameteuliwa na Tume ya Huduma za Mahakama kuchukua wadhfa wa Jaji wa Mahakama ya Juu ulioachwa wazi kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa Jaji wa mahakama hiyo, Phlip Tunoi. Hadi kuteuliwa kwake, Lenaola amekuwa Jaji wa Mahakama Kuu.
Alipohojiwa tarehe 12 mwezi huu wakati wa mchakato wa kujaza wadhfa huo, Lenaola alieleza imani yake kuwa ana tajriba ya kutosha kuwa Jaji wa Mahakana ya Juu.
Lenaola vilevile anakumbukwa kwa kauli yake kuwa iwapo angelinganishwa na mnyama angekuwa ndovu, alipoulizwa swali hilo wakati wa mchujo.