Na Rosa Agutu/Beatrice Maganga
Huku kaunti mbalimbali zikiendelea kuathiriwa na ukame, Msemaji wa Serikali, Eric Kiraithe amesema serikali imeweka mikakati kuwasaidia waathiriwa. Kiraithe amesema tayari shilingi milioni 250 zimetengwa kuwanusuru walioathirika huku serikali kuu ikiendelea kushirikiana na zile za kaunti kutafuta suluhu ya kudumu.