×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]
Premium

Magoha awaonya walimu dhidi ya kuwachapa wanafunzi

Serikali imesisitiza kwamba haitaruhusu adhabu ya vibiko dhidi ya wanafunzi katika shule za humu nchini. Waziri wa Elimu Profesa George Magoha amesema haifai walimu kuwashurutisha wanafunzi kupata alama za juu katika mitihani.

Akizungumza katika Shule ya Msingi ya Wagwer Kaunti ya Siaya, Waziri Magoha amesema mwalimu anayesemekana kumwadhibu kwa kumchapa mwanafunzi katika Shule ya Msingi ya Nyamninia atachukuliwa hatua. Magoha amesema  maafisa wa polisi na wale wa Tume ya Huduma za Walimu TSC wanashirikiana katika uchunguzi huo.

Mwalimu huyo alikamatwa jana na anatarajiwa kufikishwa mahakamani Jumatatu.

Ikumbukwe japo walimu wanaruhusiwa kuwaadhibu wanafunzi sehemu ya 29 ya katiba imepiga marufuku adhabu ya viboko shuleni.

Wakati uo huo, Magoha amewaonya walimu dhidi ya kuwahangaisha wanafunzi   kwa kutotimiza mahitaji mbalimbali yakiwemo malipo  ya masomo ya ziada akisema  serikali kupitia wizara ya elimu wamewekeza vilivyo kwa wanafunzi hao na hivyo hawafai kutumiwa nyumbani kwa sababu ya pesa.

Kuhusu ujenzi wa madarasa ili kufanikisha mpango wa mtaa wa umilisi Magoha amesema ujenzi wa madarasa yote 3, 500 unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti.

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week