Shughuli ya uhamasisho wa wapigakura inayoendeshwa na Tume ya Uchaguzi, IEBC imeingia wiki ya pili Jumatau hii.
IEBC ilizundua kampeni hiyo ya siku 18 tarehe 12 mwezi Julai kwa lengo la kuwahamasisha wapigakura kushiriki uchaguzi wa Agosti 9.
Miji mikuu inayolengwa na Kisumu, Nairobi, Nakuru na Mombasa.
Maafisa wa IEBC wakiongozwa na Mkurugenzi wa usajili na shughuli za upigaji kura Rasi Masudi, wametangamana na wananchi ili kujibu maswali kuhusu mchakato wa kupiga kura.
Hata hivyo, IEBC imechelewesha mpango huo kulinganisha na miaka ya awali ambapo kufikia Julai, Wakenya wangekuwa wamefahamishwa kuhusu uchaguzi kupitia kampeni na matangazo ya vyombo vya habari.
Tume ya IEBC imekuwa ikilalamikia ukosefu wa fedha za kuendesha shughuli zake.