×
App Icon
The Standard e-Paper
Read Offline Anywhere
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]
Premium

Tuju avunja kimya chake kuhusu madai ya Chebukati

Living

Mkurugenzi Mkuu Chama cha Azimio la Umoja One Kenya Raphael Tuju amevunja kimya chake kuhusu madai yaliyoibuliwa katika hati kiapo ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi IEBC Wafula Chebukati kwenye rufaa ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais.

Katika kikao na wanabari, Tuju ambaye amekiri kukutana na Chebukati amejitetea akisema walikutana naye akiwa na watu wengine na hivyo madai ya kuwa alilenga kushawishi matokeo ya uchaguzi ni uongo.

Tuju ambaye anasema alijaribu zaidi ya mara tatu kumwona Chebukati, alifanya hivyo baada ya kufahamishwa kuhusu kufutwa kwa fomu za 34A kwenye mtandao wa IEBC na kutundikwa kwa fomu nyingine katika wavuti huo, madai ambayo Tuju anasema aliyawasilisha kwa Idara ya Upelezi DCI. Aidha Tuju anasema jamaa aliyemfahamaisha alikuwa mfanyakazi wa IEBC ambaye alitishiwa na Afisa Mkuu Mtendaji wa IEBC Marjan Hussein Marjan, alipojaribu kumfahamisha kuhusu kubadilishwa kwa fomu hizo.

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week

.

Similar Articles

.

Recommended Articles