×
App Icon
The Standard e-Paper
Informed Minds Prefer The Standard
★★★★ - on Play Store
Download Now
×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Tobiko apinga kuachiliwa kwa mshukiwa wa ulanguzi wa dawa za kulevya

Living

Na,Sophia Chinyezi

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma, Keriako Tobiko amekata rufaa dhidi ya uamuzi wa kuamwachilia kwa dhamana raia wa Uingereza aliyeshtakiwa kwa ulanguzi wa dawa za kulevya. Tobiko anasema huenda Jack Marrian akakosa kuhudhuria vikao vya kesi dhidi yake. Mapema leo, Mahakama ya Kibera imemwachilia Jack kwa dhamana ya shilingi milioni sabini na wadhamini wawili, kwenye kesi ya ulanguzi wa dawa aina ya cocaine zenye thamani ya shilingi milioni 598. Dawa hizo zilipatikana kwenye Bandari ya Kilindini Mombasa. Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Kibera, Derrick Kuto ameagiza Marrian awe akifika katika ofisi ya mpelelezi katika kesi hiyo mara moja kila wiki. Wakati uo huo Mkenya, Roy Francis Mwanthi, ambaye anakabiliwa na mashtaka sawa hayo, ameachiliwa kwa dhamana ya shilingi milioni sitini na wadhamini wawili. Hata hivyo upande wa mashtaka umeeleza kutoridhishwa na uamuzi wa kuwaachilia wawili hao kwa dhamana na kusema watakataa rufaa.

 

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week

.

Similar Articles

.

Recommended Articles