Ishara ya mtego wa kutegana wa NASA ni dhahiri uliteguliwa punde tu baada ya Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga kukumbatiana kwa busu la mkono wa kheri, almaarufu “hendisheki”.
Uhusiano mpya baina ya Rais wa Jamhuri na kinara wa upinzani ulizika kabisa katika kaburi la sahau maazimio ya ushirikiano wa vyama vya ANC (Musalia Mudavadi) na Ford Kenya (Moses Wetangula) ambao wote hawa wanajivunia kumchangia kura za urais Raila Odinga kipindi cha uchaguzi mkuu uliopita wa 2017.