Mmoja wa familia ya Sultan wa Zanzibar na ambaye amekuwa mfalme wa miaka mingi katika himaya za kiarabu, Sultan Qaboos bin Said, binamu wa Sultan wa mwisho wa Zanzibar Jamshid bin Abdullah al Said ameaga dunia nchini Oman.
Kifo cha Sultan Qaboos kwa Wakenya chungu nzima hususan katika mwambao wa pwani ya Kwale, Mombasa, Kilifi, Malindi na Lamu ni afueni kutokana na mwamko mpya ambao mwendazake alikuwa ameanza kusukuma vizazi wa Sultan kurudi kunyang’anya ardhi wapwani ambao wamekalia ardhi ambazo Warabu wa Oman walinyakuwa awali.