Kaunti ya Mombasa ni kivutio cha utalii kutokana na bahari na mandhari safi ya kupendeza ila cha kushangaza ni kwamba Mombasa umekuwa mji ambao unazidi kutiliwa shaka kutokana na visa vya utovu wa usalama. Licha ya waziri wa usalama wa ndani Dakta Fred Matiangi kuzuru Mombasa na kutoa onyo kali na mageuzi katika idara ya usalama, magenge mapya yanaendelea kuchipuka hapa Mombasa.
Kulingana na ripoti iliyotolewa na shirika la kutetea haki za binadamu la Haki Afrika, watu 40 wameripotiwa kuuawa na magenge ya kihalifu katika kipindi cha mwaka mmoja, huku washukiwa 30 wa magenge hayo, ndio ambao wamekamatwa na maafisa wa polisi kufikia sasa.