Moyo wangu umejawa na simanzi. Nasikitishwa sana na hali ya nchi yetu. Hali hii inazidi kuzorota. Kwenye runinga na magazeti twaelezwa kwamba uchumi uko imara. Hali halisi ni tofauti kabisa! Wenyenchi wanakosa chakula cha msingi!
Unga wa ugali sasa umegeuka kuwa kumbukumbu tu kwenye vichwa vya wengi. Kipenzi cha wengi, ugali, sasa haupatikani kwa urahisi. Eti haya yote kwa kisingizio cha ukosefu wa mahindi nchini. Hadithi ya kupotea kwa mahindi na kuagizwa kwa mahindi toka nje bado twaiwazia.