Kwa kweli umbo lake halieleweki na linaashiria haswa matendo yake.Mara nyingi hana haraka wala kelele na anapoamua kutekeleza uhuni wake habahatishi. Hata hivyo, anajitia kulifahamu shamba na utamu wa nafaka kuliko mkulima mwenyewe.
Licha ya hayo, yeye hula bila kujua ni nani aliyetengeneza au kupanda. Vile vile hula kwa dharau akiharibu bila kujali juhudi zilizotumika kutengeneza chambilecho wahenga 'ukiona vyaelea vimeundwa’.