×
App Icon
The Standard e-Paper
Informed Minds Prefer The Standard
★★★★ - on Play Store
Download Now

Samboja kikapuni akielekea kwa Raila

Gavana wa Taita Taveta Granton Samboja na Kinara wa ODM Raila Odinga.

Wangwana wa kaunti ya Taita Taveta, nambari 006 kati ya kaunti 47 za Kenya wangali wamepigwa na butwaa wakati gavana wao Granton Samboja ambaye aliingia uongozini mwaka 2017 kwa tikiti ya kulazimishwa ya WIPER, alimkimbilia kiongozi wa upinzani Raila Odinga badala ya kinara wake wa chama Stephen Kalonzo Musyoka kwa ushauri wa dharura kuhusiana na kusambaratika kwa serikali yake kufuatia mjuvyo wa kiutawala baina yake na wawakilishi (MCAs) wa wadi za Taita Taveta.

Habari za kuaminika zatujia kinaga ubaga kwamba Gavana Samboja huenda akahamia rasmi kwa chama cha ODM siku chache zijazo kubwaga chama cha WIPER, tayari kwa vita vyovyote vile vya siasa ya uchaguzi mpya mdogo wa kaunti endapo pendekezo lake la kuitaka serikali ya kaunti ya Taita Taveta ivunjiliwe mbali litatimia.

Get Full Access for Ksh299/Week
Unlock the Full Story — Join Thousands of Informed Kenyans Today
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in