Licha ya serikali ya Kaunti ya Nairobi kutumia mabilioni ya fedha kwenye ujenzi wa barabara ili kupunguza msongamano wa magari jijini, wahudumu wa magari bado wanapitia changamoto si haba kuingia na kutoka jijini hali ambayo imesababisha hasara katika sekta ya uchukuzi.
Kwa mujibu wa washikadau katika sekta ya trafiki, uegeshaji wa magari katikati ya jiji unapaswa kupigwa marufuku na badala yake mabasi yanayobeba abiria wengi kutumika.