Wakenya leo hii wamemheshimu Waziri wa Usalama wa Taifa na Ushirikishi wa Serikali Kuu Dkt Fred Matiangí kama mpasua mwamba katika masuala sugu ambaye kwa njia moja au nyingine, serikali imeelekea kufikia ngamani mwa suluhisho.
Yeye ni kimbunga ambacho ukisimama mbele yake, utasombwa na kikukuzi (upepo) wake mkali wa msimamo wa kikazi. Wengi hatahivyo hawajui kwamba Matiang’I sawia na Wakenya wengi, ni mtoto wa skwota ambaye wazazi waliwajibika kuhama kutoka kwa kijishamba kidogo katika eneo la Mugirango Kusini hadi eneo bunge la Borabu Kaunti ya Nyamira wanapoishi kwa sasa.