Mpango wa kuhakikisha kuwa watahiniwa wote waliofanya mtihani wa darasa la nane, KCPE mwaka jana kujiunga na shule za upili hautafanikiwa iwapo serikali haitaimarisha miundo-msingi.
Katika hoja iliyowasilishwa bungeni na Mbunge wa Emuhaya, Omboko Milemba, serikali imeshauriwa kuhakikisha kuwa asilimia 70 ya fedha zinazotengewa hasa shule za upili za kutwa zinatengewa muundo msingi.