Chama cha KANU chamtaka Naibu wa Rais William Ruto ajiuzulu

Chama cha KANU katika Eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa kinamtaka Naibu wa Rais Dakt William Ruto kujiuzulu, na kumruhusu Rais Uhuru Kenyatta kuendeleza vita dhidi ya ufisadi nchini.

Akizungumza katika afisi za chama hicho, Mwenyekiti wa chama hicho tawi la North Rift Paul Kibet, amemtaka Ruto kujiondoa katika wadhifa huo kwa madai kuwa haungi mkono kikamilifu ajenda ya serikali kukabili ufisadi.

Kibet ameukosoa msimamo ambao umechukuliwa na baadhi ya viongozi kutoka eneo la bonde la ufa wanaomuunga mkono  Ruto, kufuatia semi za matusi yanayoelekezwa dhidi ya  Rais Kenyatta.

Ikumbukwe kuwa wiki iliyopita, viongozi wa chama cha KANU na kile cha ODM katika eneo zima la Bonde la ufa, walijitenga na matamshi ya baadhi ya wanasiasa kutoka eneo hilo ya kumkashifu Rais Uhuru Kenyatta wakidai kuwa eneo hilo limelengwa kwenye vita dhidi ya ufisadi.

Related Topics