Aliyekuwa Gavana wa Nairobi, Evans Kidero ametuhumiwa kuchangia kupotea kwa shilingi bilioni 21 za serikali ya Kaunti ya Nairobi alipokuwa akihudumu katika wadhifa huo.
Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Uhasibu la KPMG iliyokabidhiwa Gavana wa sasa, Mike Sonko masuala kadhaa yameibuliwa kukiwamo kufunguliwa kwa akaunti kisiri, kuchukuliwa kwa kodi kutumia vitabu vya risiti ambavyo haviwezi kukaguliwa na matumizi ambayo yalifanywa pasi na kutumia mfumo rasmi wa serikali wa IFMIS.