Na Carren Omae
Huku bunge la Kitaifa likisubiria kuona iwapo litatii agizo la mahakama la kulizuia kuendela kujadili ombi la kumtaka Mhasibu Mkuu wa Serikali, Edward Ouko kuondolewa ofisini huenda mjadala kuhusu suala hilo ukachukua mkondo mwingine, kufuatia madai kwamba Kamati ya Fedha Bungeni ina njama ya kumwondoa ofisini.
Madai hayo yamerejelewa leo na Ouko huku akilalamikia jinsi utaratibu wa kushughulikia ombi hilo unavyoendeshwa.
Jinsi ilivyo miongoni mwa maafisa wa serikali wanaohusishwa na sakata mbalimbali, hali kumhusu Mhasibu Mkuu wa Serikali Edward Ouko haijakuwa tofauti. Ouko amekuwa mwepesi wa kuapa kutoondoka ofisini akisema hakuna uchunguzi unaoendelea dhidi yake.